المدة الزمنية 33:12

Salama Na CHARLES HILLARY Ep 38 | MZEE WA BUSARA Part 1

بواسطة YahStoneTown
94 048 مشاهدة
0
976
تم نشره في 2020/10/17

#YAHStoneTown #SalamaNa #PodCast SUBSRIBE TO OUR CHANNEL https://bit.ly/YahStoneTownSubs Listen our Podcast on Spotify Link https://spoti.fi/2Uxr6Cm� �� ‪ApplePodcast Link https://apple.co/2Ou1bru� �� GooglePodcast Link https://bit.ly/GooglePodcastSalamaNa Audiomack Link https://bit.ly/YahStoneTownAudioMack ‪YouTube Link http://bit.ly/YoutubeSalamaNa Ilinichukua muda mrefu kuweza kupata nafasi ya kuongea uso kwa macho na Charles Hillary, maana toka enzi za Mkasi nilikua natafuta mwanya wa kuweza kukaa nae chini walau kwa hata nusu saa tu. Sikuwahi kukata tamaa badala yake nilikua kama chui kwenye mawindo yake, na mwisho wa siku kwa uwezo wa Mungu, binti yake Faith, Ivona Kamuntu na Mama kule nyumbani waliniwezesha kushinda mechi hii hatimaye. Mungu anajua tabasamu lilikua la ukubwa wa kiasi gani, na pengine hilo linaweza likawa limefanya niwe excited sana mpaka mengine nikayasahau kuyauliza, au kujua naulizaje, au kushangaa sana? Ushawahi kukutana na mtu alafu ukasahau yote ulotaka kuyasema, au kufanya. Ukabaki tu umeganda kama sanamu? Bado? Basi we ngoja tu. Simkumbuki Charles Hillary wa Radio Tanzania (RTD), namkumbuka wa Radio One zaidi. Wa taarifa ya habari, wa kipindi cha charanga, wa kutangaza mpira, huyo ndo ambaye alinifanya mimi nipende Radio, nipende kuskiliza mpira na pengine kuutangaza. Sauti yake tamu na lafdhi ilonyooka ilikua inakufanya uone kama unaona haswa anachokiongea. Kipaji cha kipekee kabisa. Kipaji kutoka kwa Mwenyezi Mungu ambacho pia kilihitaji kujituma na kujitetea na kujiamini sana. Kutimiza ndoto si suala la kulala na kuamka tu, suala la kukosa usingizi. Suala la kutokwa na jasho, suala la kulia kwasababu tu unadhani hakuna anaye skiliza mawazo yako na ndoto zako... Mpango ni kutokata tamaa kamwe! Hayo ni baadhi tu ya mambo ambayo yeye alipitia na akaja akawa Lejendari huyu tumpendaye na kumheshimu wote. So nlitaka kumfahamu zaidi, na huwezi kumfahamu mtu kama hujauliza maswali, so tulianzia kwenye asili yake na elimu, na kwa Mama yake ana Baba yake, kwenye kazi yake ya kwanza, vipindi vigumu katika maisha yake, transfer za kazi. Pia jinsi alivyokutana na Mama wa watoto wake, na zaidi tulimzungumzia Mama wa mtoto wake wa pili, wa kwanza hatukumzungumzia, skuona sababu ya kufanya hivyo maana alikua excited zaidi kumuongelea Sarah, ambaye anampikia wali na njegere zilizonyooka zaidi dunia nzima 😄. So alikutana naye vipi? Mwaka gani? Pia tuliongea kuhusu teknolojia na jinsi ambavyo yeye anaenda na wakati. Mahusiano yake na Ivona Kamuntu na AzamTV kwa ujumla. Kama nilivyosema mwanzo wa story yangu hii na Charles Hillary, naomba ufahamu kwamba hii ni moja ya interview nilizokua natamani kufanya na natumai pia uta enjoy na pia utajifunza chochote kitu kwenye suala zima la utafutaji, malezi, ndoto na mipango maana binafsi nimechota kadhaa. Lejendari akija mezani unachotakiwa kufanya ni kuskiliza zaidi na kuongea kidogo. Enjoy. Love, Salama. Soundtrack Yeah by @MarcoChali /watch/QLnf4BH1euC1f Follow: Twitter: http://twitter.com/YahStoneTown Instagram: http://Instagram.com/YahStoneTown Facebook: http://facebook.com/YahStoneTown

الفئة

عرض المزيد

تعليقات - 174