DAR: BASI LA MWENDOKASI LAGONGANA NA PIKIPIKI, WAWILI WAFARIKI
-
Kamanda wa Polisi kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumnne Muliro amesema Septemba 8, saa tatu usiku basi la mwendo kasi liligongana na pikipiki na kusababisha vifo vya watu wawili
-
Ajali hiyo ilitokea barabara ya mwendokasi eneo la Lumbumba kwenye taa za kuongoza magari. Chanzo cha ajali hiyo imetajwa kuwa ni dereva wa pikipiki kujaribu kupita wakati taa nyekundu imewaka
-
Waliofariki ni Sami Riyaz Khan (17), aliyekuwa dereva na abiria wake Patrick Chohan(16). Wito umetolewa kwa madereva wa pikipiki kutii sheria na kuvaa kofia ngumu